|
|
|
VIDEO - Drogba Aizamisha Arsenal |

Thomas Vermaelen wa Arsenal kushoto akiwania mpira na Didier Drogba wa Chelsea |
Monday, February 08, 2010 2:26 AM
Nyota wa Ivory Coast, Didier Drogba ameendeleza rekodi yake nzuri ya kuwatungua Arsenal kwa kuifungia Chelsea mabao yote mawili katika kichapo cha mabao 2-0 walichowapa vijana wa Arsene Wenger na kulifanya pengo la pointi kati ya Chelsea na Arsenal kufikia pointi 9. VIDEO ya magoli yote katika mechi hii mwisho wa habari. |
Matumaini ya Arsenal kutwaa kombe la ligi kuu ya Uingereza yamezidi kufifia baada ya kupokea kipigo cha pili mfululizo katika ligi ya Uingereza.
Wiki iliyopita Arsenal ilibamizwa 3-1 na mashetani wekundu wa mji wa Manchester, Manchester United na wiki hii imekubali kupokea kipigo kingine cha mabao 2-0 toka kwa Chelsea.
Drogba ambaye ana rekodi nzuri ya kuzifumania nyavu za Arsenal kila Arsenal inapokutana na Chelsea, ndiye aliyeifungia Chelsea mabao yote mawili katika ushindi wa leo katika uwanja wa Stamford Bridge.
Arsenal ilicheza vizuri zaidi kwenye kipindi cha pili na kulisakama sana lango la Chelsea lakini washambuliaji wake walishindwa kulipenya lango la Chelsea lililoongozwa na nahodha John Terry.
Kwa ushindi wa leo, Chelsea imejikita kileleni mwa ligi ya Uingereza ikiwazidi Manchester United wanaoshika nafasi ya pili kwa pointi mbili.
Chini ni VIDEO ya magoli yote katika mechi hii. |
|
|
VIDEO - Chelsea 2-0 Arsenal
Na Mohamed Kindindi, Uingereza
|
|
|
|
|
|
|
|
Mtoa Maoni:
Nyoshi
Monday, February 08, 2010 03:22:21
|
|
Mtoa Maoni:
KING
Monday, February 08, 2010 09:06:21
|
|
Mtoa Maoni:
zhao
Monday, February 08, 2010 09:50:28
|
|
Mtoa Maoni:
Great Thinker
Monday, February 08, 2010 15:58:01
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Habari zaidi za michezo |
...Habari Zaidi
|
|
Advertisements

|
|
Habari Zilizosomwa Sana |
|
|
|
|
| Photo Gallery |
 |
|
|
 |
|
|
|
|
|
|
|