Tangaza Hapa Email: sales@nifahamishe.com
   
 
Member's Login
Username
Password
Not a member? Sign Up
            Sign Out

 
 
John Terry Anyang'anywa Unahodha Baada ya Kumtia Mimba Shemeji Yake


John Terry
Friday, February 05, 2010 9:50 PM
Kocha wa timu ya taifa ya soka ya Uingereza, Fabio Capello amemnyang'anya unahodha John Terry kufuatia skendo lake la kumtia mimba mpenzi wa mchezaji mwenzake na kisha kuitoa mimba hiyo.
Skendo la John Terry kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mpenzi wa mchezaji mwenzake wa timu ya taifa ya Uingereza limefikia hatua nyingine kwa kocha wa Uingereza kumvua unahodha John Terry.

John Terry ambaye ana mke na watoto wawili anashutumiwa kumzunguka rafiki yake Wayne Bridge ambaye walicheza pamoja Chelsea na kutembea na mpenzi wake mrembo wa Ufaransa, Vanessa Perroncel.

Mbali ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Vanessa ambaye amezaa mtoto mmoja na Wayne Bridge, Terry anadaiwa kumtia mimba Vanessa na kisha kuitoa mimba hiyo ili siri ya uhusiano wao isifichuke.

Terry alianza uhusiano na Vanessa mwaka jana baada ya Wayne Bridge kuhama Chelsea ya London na kuhamia mjini Manchester kuichezea Manchester City.

John Terry anacheza nafasi ya kati ya ulinzi katika timu ya taifa ya Uingereza wakati Wayne Bridge naye yumo kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza akicheza kama beki wa kushoto.

Akiliongelea suala hilo leo mchana, kocha wa Uingereza raia wa Italia, Fabio Capello alisema kuwa ili kuikoa timu ya taifa ya Uingereza isifanye vibaya kwenye kombe la dunia, ameona ni bora amnyang'anye unahodha John Terry.

Vyombo vya habari vya Uingereza vililishikilia bango skendo la Terry na kutaka anyang'anywe unahodha lakini chama cha soka cha Uingereza kilisema kuwa uamuzi wa mwisho atautoa Capello.

Capello ameamua kumchagua Rio Ferdinand kuwa nahodha mpya wakati Steven Gerrard atakuwa nahodha msaidizi.

 
    
Mtumie Rafiki Yako
  Comments    Add your Comment

Mtoa Maoni: zhao    Friday, February 05, 2010 22:55:18   
 
bab terry usijali kwanza hawawezi kukuacha hao kuntu,na nyinyi wanawake mnababaika na mstaa kina UBUGUVU na momso wao wanang'ara kwa kucheza kobole
 
 
Mtoa Maoni: Semenya    Friday, February 05, 2010 23:30:37   
 
Heh!! kumbe kina ZUMA nao wapo ulaya!!!
 
 
Mtoa Maoni: Great Thinker    Saturday, February 06, 2010 01:00:51   
 
Never mind Terry, you are the star and Fabio Capello will never leave you out of the England squad for the forthcoming World cup. I'm cofident you will show your quality in South Africa. All the Best John in your carrier!
 
 
Mtoa Maoni: Mutalemwa    Saturday, February 06, 2010 17:40:55   
 
Kama bongo hakuna kunyanganywa kitu, hayo mambo yao wenyewe, kina Terry wangapi bongo wanapeta tu, kutuchukulia wake zetu
 
 
Mtoa Maoni: KING    Saturday, February 06, 2010 19:53:46   
 
Football politics.................what has it to do with ground performance? England wanajichimbia kabuli la failure ktk World cup kwa mitafaluku hii ya kidaku.
 
 
       Jumla kuna maoni (6), Soma maoni yote
Unakaribishwa kuchangia maoni yako
Jina Lako    *
Maoni Yako *
 
*** Unaruhusiwa kutuma maoni yako yoyote yale. Tafadhali tumia lugha nzuri, maoni yenye kukashifu watu na yasiyofaa kwa jamii hayataruhusiwa. ***

*** Maoni yanayotolewa hapa ni mawazo binafsi ya Mtoa Maoni
Nifahamishe.com Haihusiki na maoni yatakayotolewa ***
Habari zaidi za michezo
> Ligi Kuu Bara Kuanza Jumamosi, Waamuzi Acheni Unazi
> Kenneth Asamoah Boateng: Mtambo mpya wa mabao Yanga
> 'Huu Ndiyo Uchawi Wangu' - Fuso
> Kaseja na Kado Wachuana Kuwania Jezi Namba 1
> Kocha Mpya Stars Aguswa na Kiwango cha Ngasa
> Nyota wa Uingereza Amhonga Kahaba Paundi 800 Kwa Usiku Mmoja
> Taifa Stars Kujipima Ubavu na Wamisri
> VIDEO - Ushangiliaji wa Goli Ambao Haujawahi Kutokea
> Baada ya Kubugizwa 6-0 Twiga Stars Yaja na Visingizio Kibao
> Ngassa Kizani Azam Fc
> Simba Yaiovateki Yanga na Kumsajili Gumbo
> Jeuri ya Wachina Bongo
> Kocha Wa Yanga Hataki Masihara
> Matumla Ajigamba Kumdunda Maugo
> Semenya Arudi Kwenye Riadha Kwa Ushindi
> VIDEO - Ajaribu Kuliiba Kombe la Dunia
> VIDEO - Hispania Wawa Mabingwa Wapya wa Dunia
> Wachezaji wa Hispania Waingizwa Mjini Afrika Kusini
> Sweta la Bluu Ndilo Linaloipa Ushindi Ujerumani
> Wawili Wauliwa Kenya Kwasababu ya Mechi ya Ghana
> Ghana Yawasononesha Waafrika
> Brazil Chariii!! Yatolewa Kombe la Dunia
> Ujerumani Yaicharanga Uingereza 4-1
> Ivory Coast Yaliaga Kombe la Dunia, Ghana Ndio Tegemeo Lililobaki
> Ghana Yaibeba Afrika, Algeria Yafungashwa Virago

...Habari Zaidi

 

Advertisements
Namabengo Computer Repairing Services Call: 0762-486583 0r 0712-409641
Habari Zilizosomwa Sana
1 'Yesu Alikuwa ni Muathirika w...
Photo Gallery
Photo Album

 Ukisikia Wazazi bomu
Random Photo

 Ashakum
Habari Mpya Mpya
> 'Yesu Alikuwa ni Muathirika wa Ukimwi'
> PICHA - Mapenzi Yanaua..
> Askofu Awaponda Wanaomtukana Kikwete
> Siri ya Kimada Yafichuka
> Ajinyonga Baada ya Kunyimwa Mkopo
> VIDEO - Mwanaume Anayemchezea Simba Sharubu
> Kampeni zachachamaa, wapinzani nao watoa ahadi
> JK aendelea kutoa ahadi
> Pingamizi la Chadema baada ya siku 5
> Urefu Wasababisha Aache Shule ya Msingi